![]() |
| Ndugu Gerald Bundala, Rais mteule wa UDOMSSO |
Jumuia ya wanafunzi wanaosoma sociology katika chuo kikuu cha Dodoma (UDOMSSO) imepata viongozi wapya wa kuiongoza jumuia hiyo kubwa ya wanafunzi chuoni hapo. Mchakato wa kupata viongozi wapya ulianza wiki mbili kabla ya tarehe ya uchaguzi ambapo wagombea walijitokeza kuchukua form za kugombea katika nafasi tofauti tofauti.
Katika uchaguzi huo uliofanyika tarehe 10/6/2017, viongozi kadhaa waliweza kutangazwa kuwa washindi wa nafasi walizokuwa wakiwania katika kuiongoza jumuiya hii. Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi hiyo Bwana Edward Mdaki kwa kushirikiana na wanatume wengine Luciana Daudi, Msafiri Ponera na Ally Hafidh katika kusimamia uchaguzi huo; alimtangaza Bwana Gerald Bundala aliyekuwa Katibu Msaidizi wa jumuiya hiyo katika awamu iliyopita kuwa Rais mpya wa UDOMSSO. Aidha nafasi ya Rais msaidizi alichaguliwa
