![]() |
| Tundu Lisu |
Tukio
la kupigwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Antipas Lissu (Chadema) na
watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwake jana mchana limeendelea kulaaniwa
vikali na watu mbalimbali wakiwemo wanasiasa, viongozi wa dini na wananchi
mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii na media nyinginezo.
Lissu akiwa amefika nyumbani kwake Area D, eneo la Site Three, baada ya
kuahirishwa kwa kikao cha bunge, kabla hajashuka kwenye gari watu wasiojulikana
wakiwa kwenye gari linalodaiwa kuwa ni aina ya Nisani ambalo namba zake
hazikutambulika, walianza kumshambulia kwa risasi.
Kwa mujibu wa ripoti ya Kamanda wa Polisi Dodoma, Gilles Muroto,
risasi



