Msikilize hapa alichokizungumza Mbunge wa Siha kupitia CHADEMA Dr. Molel mara baada ya kujiuzulu nafasi ya ubunge na kujiunga na CCM. Ikumbukwe ni siku chache tu baada ya mbunge wa Kinondoni kupitia CUF (Maulid Mtulia) kujiuzulu na kuhamia CCM. Ni katika mfululizo wa Viongozi na wakereketwa mbalimbali kutoka vyama vya upinzani kuvihama vyama vyao na kujiunga na chama tawala cha CCM.
ABOUT UDOMSSO
The University of Dodoma Sociology Students' Organization (UDOMSSO) is an academic and social organization which is under the department of Sociology and Anthropology in the College of Humanities and Social Sciences.
MISSION
Our mission is to Organize, Coordinate and Facilitate all activities relating to our areas of interest for social progress.
VISSION
UDOMSSO has a vission to become an effective students' organization and to spearhead for a positive community for both academic and social matters which affect students' daily life and the community at large.
Translate
Thursday, 14 December 2017
MAGUFULI AGOMA KUZIKWA DODOMA, ARUDISHA ARDHI KWA WANANCHI.
Rais Magufuli amerudisha ardhi yenye ukubwa wa zaidi ya ekali 100 kwa wananchi mjini Dodoma na kusema kuwa yeye atakapokufa asizikwe mjini Dodoma. Eneo hilo lilitengwa na serikali kwa ajili ya maziko ya viongozi mjini hapo lakini viongozi wengi wamekuwa wakipendelea zaidi kuzikwa kwao. Magufuli ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa nyumba za Iyumbu mkoani Dodoma."Mimi nimeshasema nikifa nazikwe kule nyumbani alikozikwa....
Saturday, 9 December 2017
BABU SEYA NA MWANAE WAPATA UHURU SIKU YA UHURU.
![]() |
| Babu Seya akiwa na mwanaye Papii Kocha |
Shangwe na nderemo vimesikika kutokakwa Watanzania walio maeneo tofauti tofauti ya nchi ya Tanzania hususani waliokuwepo ndani ya uwanja wa Jamhuri yalipo makao makuu ya Tanzania Dodoma na wale waliokuwa majumbani wakifuatilia sherehe za kuadhimisha miaka 56 ya kupatikana kwa Uhuru wa Tanganyika uliopatikana tarehe 9/12/1961. Shangwe hizo kubwa zilitokana na kauli ya mgeni rasmi katika sherehe hizo ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mheshimiwa Dk. John Pombe Magufuli ambaye mbali na kusamehe wafungwa 8157 leo
Friday, 8 September 2017
TUNDU LISU AHAMISHIWA NAIROBI, AFYA YAKE INATIA MOYO
![]() |
| Tundu Lisu |
Tukio
la kupigwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Antipas Lissu (Chadema) na
watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwake jana mchana limeendelea kulaaniwa
vikali na watu mbalimbali wakiwemo wanasiasa, viongozi wa dini na wananchi
mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii na media nyinginezo.
Lissu akiwa amefika nyumbani kwake Area D, eneo la Site Three, baada ya
kuahirishwa kwa kikao cha bunge, kabla hajashuka kwenye gari watu wasiojulikana
wakiwa kwenye gari linalodaiwa kuwa ni aina ya Nisani ambalo namba zake
hazikutambulika, walianza kumshambulia kwa risasi.
Kwa mujibu wa ripoti ya Kamanda wa Polisi Dodoma, Gilles Muroto,
risasi
DOGO MTEKAJI WA WATOTO AUAWA AKIJARIBU KUWATOROKA ASKALI.
![]() |
| Peter Samson, Mtuhumiwa wa utekaji wa watoto |
Akizungumza
na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha,
Charles Mkumbo alisema Peter aliuawa na askari polisi wakati akijaribu
kuwatoroka eneo la Mkonoo, Kata ya Muriet jijini Arusha.
Peter Samson mwenye umri wa miaka 18 ni dogo kiumri lakini ni mtuhumiwa
wa vitendo vya utekaji wa watoto jijini Arusha. Kijana Peter ambaye imebainika
alikuwa akiishi na kaka yake ambaye ni askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia
(FFU) mkoani Arusha, ameuawa wakati
NI MADINI TENA! HAYAJAMWACHA MTU SALAMA!
![]() |
| Waziri Simbachawene |
![]() |
| Madini ya Tanzanite |
Ripoti za kamati za uchunguzi wa biashara ya
madini ya Tanzanite na Almasi zilizoundwa na spika wa Bunge Job Ndugai ziliwasilishwa
na Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano ndugu Kassim Majariwa mikononi mwa rais
Magufuli jana Ikulu jijini Dar es salaam. Ripoti hizo zimewataja baadhi ya
viongozi wa Serikali akiwemo Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, James
Mdoe; Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene na Naibu Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi, Mawasiliano Edwin Ngonyani na wengine.
Baada ya kupokea ripoti hiyo,
Sunday, 25 June 2017
UDOMSSO YAPATA VIONGOZI WAPYA
![]() |
| Ndugu Gerald Bundala, Rais mteule wa UDOMSSO |
Jumuia ya wanafunzi wanaosoma sociology katika chuo kikuu cha Dodoma (UDOMSSO) imepata viongozi wapya wa kuiongoza jumuia hiyo kubwa ya wanafunzi chuoni hapo. Mchakato wa kupata viongozi wapya ulianza wiki mbili kabla ya tarehe ya uchaguzi ambapo wagombea walijitokeza kuchukua form za kugombea katika nafasi tofauti tofauti.
Katika uchaguzi huo uliofanyika tarehe 10/6/2017, viongozi kadhaa waliweza kutangazwa kuwa washindi wa nafasi walizokuwa wakiwania katika kuiongoza jumuiya hii. Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi hiyo Bwana Edward Mdaki kwa kushirikiana na wanatume wengine Luciana Daudi, Msafiri Ponera na Ally Hafidh katika kusimamia uchaguzi huo; alimtangaza Bwana Gerald Bundala aliyekuwa Katibu Msaidizi wa jumuiya hiyo katika awamu iliyopita kuwa Rais mpya wa UDOMSSO. Aidha nafasi ya Rais msaidizi alichaguliwa
Thursday, 18 May 2017
FUMANIZI LA WANAFUNZI LASABABISHA TAHARUKI UDOM
Wasichana wawili wanafunzi wa UDOM wamesababisha watu kuzizima kwa kelele na miruzi iliyoambatana na zomeazome baada ya kutaka kutoana ngeu kwa kile kilichotajwa kuwa ni mapenzi. Akina dada hao wakazi wa block 1 college ya Humanities wamejikuta katika kasheshe hilo baada ya kugundua kuwa wanamtumikia Bwana mmoja kinyume na mategemeo yao. Wapasha habari wa tukio hilo wanadai kuwa; Akiwa anajiamini na bila kujua, mmoja wa wanafunzi hao amefika hostel block 6 ambayo inakaliwa na wanaume kwa lengo la kumtembelea mwenzie (mpenzi wake) lakini akastaajabu kumkuta akiwa na msichana mwingine katika mazingira yaliyomtia wasiwasi na kuhisi anaibiwa. Aidha, aliyekutwa naye alijikuta akistaajabu tukio hilo kwani aliamini yuko sehemu salama na peke yake. Uzalendo ulipowashinda walianza kumiminiana maneno makali makali huku
Tuesday, 16 May 2017
WANAFUNZI UDOM WALITEMBELEA BUNGE.
Jumuia ya wanafunzi wanaosoma sosholojia katika chuo kikuu cha Dodoma (UDOMSSO) wamefanya ziara yao Bungeni ambapo walihudhuria katika kikao cha asubuhi kwanzia saa tatu. Ziara hiyo ambayo ilikuwa na wanafunzi zaidi ya 30 ilipangwa na viongozi wa Jumuiya hiyo na baadhi ya wanafunzi wa shahada ya kwanza kuanzia mwaka wa kwanza hadi wa tatu walihudhuria.
YANGA YATWAA UBINGWA KWA MARA YA TATU MFULULIZO
Klabu ya soka ya Yanga ya Dar es salaam leo imetwaa ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara kwa mara ya tatu mfululizo baada ya kuifunga klabu ya Toto African ya Mwanza kwa goli moja bila majibu. Mchezo huo uliopigwa uwanja wa Taifa, zilishuhudiwa timu zote zikicheza soka zuri huku kila mmoja akitambua umuhimu wa mechi hiyo. Wakati Yanga wakitaka kujihakikishia ubingwa, Toto African wao walikuwa wakipambana kufa na kupona ili kuhakikisha wanasalia katika
Tuesday, 9 May 2017
TEMBO WAVAMIA UDOM
Katika hali ya kukashangaza alfajiri ya leo Tembo wamevamia katika maeneo ya chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) na kuzua wasiwasi miongoni mwa wanafunzi na jamii zinazokizunguka chuo hicho. Wakati wakijiandaa kwenda madarasani, baadhi ya wanafunzi walishangaa kuona kundi la tembo wanne wakiwa wanazunguka zunguka katika vichaka vilivyopo maeneo ya UDOM jirani kabisa na hostel za wanafunzi na kutoa taarifa kwa wanafunzi wengine na hivyo kutokea kundi kubwa la wanafunzi waliokuwa wakiwatazama kwa mbali huku wengine wakihofia kuwa tembo hao wanaweza wakazivamia hostel na kuwadhuru wanafunzi au
Monday, 8 May 2017
VILIO NA SIMANZI VYATAWALA WAKATI WA KUAGA MIILI YA WANAFUNZI WA LUCKY VICENT. MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU AWAONGOZA WATANZANIA KATIKA KUIAGA MIILI YA WANAFUNZI HAO.
Hatimaye miili ya wanafunzi wa shule ya Lucky Vicent waliopoteza maisha kufuatia ajari mbaya sana ya gari iliyokuwa imewabeba wamezikwa. Wanafunzi hao 32, waalimu wawili na dereva wa gari hiyo wameagwa kwa pamoja katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha tukio lililohudhuliwa na idadi kubwa ya waombolezaji.
![]() |
| Miili ya wanafunzi 32, Walimu 2 na dereva 1 ikiwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid kwa ajili ya kuombewa na kuagwa |
endelea......
Tuesday, 2 May 2017
KUFUATIA KUFUNGA NDOA MARA YA PILI; FLORA MBASHA ANAZINI? HUU HAPA WAWEZA KUWA UKWELI.
Pamoja
na kwamba kwa sasa hapendi kuitwa jina la Flora Mbasha na kupendelea aitwe
Madam Flora, ni ukweli usiopingika kwamba wengi watashindwa kuelewa
unamzungumzia nani ukitaja Madam Flora bila kumalizia Mbasha na pengine wapo
watakaofikiri kwamba unamzungumzia mtu mwingine maarufu kama yule wa kipindi
cha Flora show kenye luninga.
Mfuatano wa majina hayo mawili unajenga picha
halisi ya mwanadada huyo maarufu Tanzania na nje ya Tanzania kwa nyimbo za
injiri zinazowagusa wengi kama vile Jipe Moyo, Maisha ya ndoa, Alionewa Yesu,
Unifiche, Fanya njia, Tanzania nakupenda, na nyingine nyingi. Licha
ya umaarufu wake katika nyimbo za injiri, Flora Mbasha ametikisa vichwa vya
watu na ku-make headlines za kutosha katika magazeti mbalimbali Tanzania na
mitandao ya kijamii kutokana na mtikisiko ulioikumba ndoa yake na mumewe wa
awali Emmanuel Mbasha. Mtikisiko huo haukuiacha ndoa hiyo salama kwani uliweza
kusababisha ndoa hiyo kuvunjika mahakamani na kila mmoja kushika hamsini zake
kama wasemavyo vijana mtaani. Pamoja na mengine yanayoweza kuwa sababu ya ndoa
hiyo kuvunjika lakini neno usaliti kwa maana ya uzinzi umezungumzwa sana kwenye
magazeti na mitandao ya kijamii kuwa chanzo kikubwa cha ndoa hiyo kuvunjika
wakihusishwa watu tofauti tofauti huku Askofu Josephat Gwajima akiangaziwa
zaidi na watu mbalimbali.
![]() |
| Flora akifunga ndoa na mumewe mpya Daudi Kusweka |
Emmanuel
Mbasha kwa wakati wake alikaririwa na watu akimtuhumu mkewe Flora kwa kumsaliti
kwa Gwajima huku Flora akikaririwa pia kumtuhumu
Saturday, 29 April 2017
UDOMSSO YAZINDUA RASMI BLOG YAKE.
Jumuia ya wanafunzi wanaosoma Sosholojia katika chuo kikuu cha Dodoma (UDOMSSO) leo wamezindua Blog hii na kuiweka rasmi katika mfumo ambao kila mtu anaweza kusoma kilichochapishwa katika Blog hii (Public readers).
Uzinduzi huo umefanyika katika mkutano mkuu (general assembly) wa wanafunzi wote wanaosoma sosholojia katika chuo kikuu cha Dodoma katika ukumbi wa theatre one, skuli ya humanities na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa jumuia hiyo pamoja na wanafunzi kuanzia mwaka wa kwanza, hadi wa tatu wanaosoma shahada ya kwanza ya sosholojia. Mkutano huo pia uliweza kuhudhuliwa na Mkuu wa Idara ya Sosholojia na Anthropolojia Dokta Nelson Ishengoma....endelea..
![]() |
| Mkuu wa Idara ya sosholojia Dr. Ishengoma akizindua rasmi Blog ya UDOMSSO na kuiweka "Public" |
Uzinduzi huo umefanyika katika mkutano mkuu (general assembly) wa wanafunzi wote wanaosoma sosholojia katika chuo kikuu cha Dodoma katika ukumbi wa theatre one, skuli ya humanities na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa jumuia hiyo pamoja na wanafunzi kuanzia mwaka wa kwanza, hadi wa tatu wanaosoma shahada ya kwanza ya sosholojia. Mkutano huo pia uliweza kuhudhuliwa na Mkuu wa Idara ya Sosholojia na Anthropolojia Dokta Nelson Ishengoma....endelea..
Tuesday, 18 April 2017
WANAFUNZI UDOM WATOA MSAADA HOSPITALI YA MKOA DODOMA
| Dr. Leah (kushoto) Mshauri katika kitengo cha damu salama na mwenzake wakiwa wamebeba boksi lenye vifaa vilivyotolewa na UDOMSSO. |
| Rais wa UDOMSSO Mr. James Simon (kulia) akikabithi moja ya boksi zenye vifaa vya matibabu vilivyotolewa na UDOMSSO. |
Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na Blood bags, Nasal Gastric Tubes na Blood giving sets ambavyo...
Thursday, 13 April 2017
KISA CHA KWELI: HUYU NDO MBWA MWENYE UPENDO WA DHATI KULIKO WANYAMA NA WATU WENGI
Anaitwa HACHIKO, ndiye mbwa anayeaminiwa kuwa na upendo
wa dhati na mtiifu kuliko mbwa wengine duniani. Alizaliwa Novemba 10, 1923
nchini Japan katika jiji la Tokyo. Umaarufu wake duniani ulitokana na heshima, upendo
wa dhati na utii kwa Bosi wake Hidesaburo Ueno aliyekuwa Profesa katika idara
ya kilimo katika chuo kikuu cha Tokyo nchini Japan.
Hachiko enzi za uhai wake |
Kila mara Hachiko alikuwa akimsindikiza Bosi wake katika kituo cha treni cha
Shibuya (Shibuya station) alipokuwa akipanda treni na kuelekea kazini. Mbwa
huyo alihakikisha Profesa Hidesaburo amepanda treni na kuondoka ndipo na yeye
anarudi nyumbani. Tofauti na wengi tusiozingatia muda; kila ilipofika jioni,
Hachiko aliwahi stesheni kumpokea Bosi wake katika kituo cha Shibuya kwani
alijua vyema muda wa treni kuwasili. Alifanya hivyo kila siku ambayo Bosi wake
alitoka kwenda kazini na kuzidi kujizolea umaarufu. Siku moja mwezi Mei 1925
alimsindikiza Bosi wake stesheni ya Shibuya kama kawaida yake bosi alipokuwa
akienda kazini. Jioni kama ilivyokuwa ada aliwahi stesheni kumpokea. Hata hivyo
treni ilipowasili,.....
Sunday, 9 April 2017
Saturday, 8 April 2017
FIRST YEAR 1 - 1 SECOND with THIRD YEAR.
![]() |
| Some Sociologist players (first year to third year) enjoying together with fans after a match |
The
First Year team was the first to score a goal through their talented striker
Kamugisha Gibson in the first half of the game before a threatening
Midfielder and a captain of General Sociologists team Charles Mwalusamba
equalizes by scoring a good goal. Up to the end of the first half, the score
board was showing 1-1.
The second half started with a tension to all players who were hardly making effort to make their team wins the game but none of them was able to score a second goal. All goalkeepers played their part effectively but the third and second year goalkeeper Yuko Mwakyusa...
Subscribe to:
Posts (Atom)
















