![]() |
| Waziri Simbachawene |
![]() |
| Madini ya Tanzanite |
Ripoti za kamati za uchunguzi wa biashara ya
madini ya Tanzanite na Almasi zilizoundwa na spika wa Bunge Job Ndugai ziliwasilishwa
na Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano ndugu Kassim Majariwa mikononi mwa rais
Magufuli jana Ikulu jijini Dar es salaam. Ripoti hizo zimewataja baadhi ya
viongozi wa Serikali akiwemo Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, James
Mdoe; Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene na Naibu Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi, Mawasiliano Edwin Ngonyani na wengine.
Baada ya kupokea ripoti hiyo,
Rais Magufuli
amewataka wateule wake wote waliotajwa katika ripoti za kamati zilizotathmini
mfumo wa uchimbaji, usimamizi, umiliki na udhibiti wa madini ya tanzanite na
almasi kukaa pembeni kupisha vyombo vya ulinzi na usalama kufanya kazi zake.
Katika kutii agizo la Rais Magufuli;Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, George Simbachawene
ameandika barua ya kujiuzulu wadhifa huo baada ya kutajwa katika ripoti za
uchunguzi wa biashara ya madini ya Tanzanite na Almasi iliyoonyesha namna
serikali lilivyopoteza matrilioni ya fedha kutokana na sababu mbalimbali.
Aidha, Simbachawene amedai kuwa ametajwa kuhusika
kwakuwa alikuwa ni mmoja wa watendaji na hivyo ni kama ajari tu lakini hakuwa
na lengo la kuihujumu nchi wala kuiletea nchi hasara iliyotajwa katika ripoti
hiyo. Magufuli ameagiza kukamatwa kwa watakaobainika na kulitia ama kulisababishia
taifa na wachukuliwa hatua za kisheria.


No comments:
Post a Comment