![]() |
| Peter Samson, Mtuhumiwa wa utekaji wa watoto |
Akizungumza
na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha,
Charles Mkumbo alisema Peter aliuawa na askari polisi wakati akijaribu
kuwatoroka eneo la Mkonoo, Kata ya Muriet jijini Arusha.
Peter Samson mwenye umri wa miaka 18 ni dogo kiumri lakini ni mtuhumiwa
wa vitendo vya utekaji wa watoto jijini Arusha. Kijana Peter ambaye imebainika
alikuwa akiishi na kaka yake ambaye ni askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia
(FFU) mkoani Arusha, ameuawa wakati
alipojaribu kuwatoroka polisi eneo la
Mkonoo jijini Arusha.
Aliuawa na Jeshi la Polisi jana, akiwa chini ya ulinzi wakati
alipokwenda kuwaonesha askari alipo mtuhumiwa mwingine waliyeshirikiana kuteka
watoto kadhaa na wengine wawili kufa kwa kuwatumbukiza ndani ya shimo la maji
taka.
“Samson alijaribu kutoroka kabla ya kuonesha mtuhumiwa mwenziwe, lakini
polisi wetu walikuwa imara walimpiga risasi miguu yote miwili na kufariki".Kamanda Mkumbo alisema Peter alitoa ushirikiano kwa Polisi na kuamua kwenda kuwaonesha mshirika mwenzake lakini kabla hawajafika eneo husika na kuonesha mshirika mwenzake ghafla alitaka kuwatoroka polisi hao na ndipo walipoamua kumpiga risasi miguu yote miwili na kumkamata kisha kumkimbiza hospitali ya Mount Meru ambapo uamauti ullimkuta.

No comments:
Post a Comment