ABOUT UDOMSSO

The University of Dodoma Sociology Students' Organization (UDOMSSO) is an academic and social organization which is under the department of Sociology and Anthropology in the College of Humanities and Social Sciences.

MISSION

Our mission is to Organize, Coordinate and Facilitate all activities relating to our areas of interest for social progress.

VISSION

UDOMSSO has a vission to become an effective students' organization and to spearhead for a positive community for both academic and social matters which affect students' daily life and the community at large.

Translate

Saturday, 29 April 2017

UDOMSSO YAZINDUA RASMI BLOG YAKE.

Jumuia ya wanafunzi wanaosoma Sosholojia katika chuo kikuu cha Dodoma (UDOMSSO) leo wamezindua Blog hii na kuiweka rasmi katika mfumo ambao kila mtu anaweza kusoma kilichochapishwa katika Blog hii (Public readers). 
Mkuu wa Idara ya sosholojia Dr. Ishengoma akizindua rasmi Blog ya UDOMSSO na kuiweka "Public"

Uzinduzi huo umefanyika katika mkutano mkuu (general assembly) wa wanafunzi wote wanaosoma sosholojia katika chuo kikuu cha Dodoma katika ukumbi wa theatre one, skuli ya humanities na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa jumuia hiyo pamoja na wanafunzi kuanzia mwaka wa kwanza, hadi wa tatu wanaosoma shahada ya kwanza ya sosholojia. Mkutano huo pia uliweza kuhudhuliwa na Mkuu wa Idara ya Sosholojia na Anthropolojia Dokta Nelson Ishengoma....endelea..

Mwenyekiti wa UDOMSSO  ndugu James Simon
Akiongea mbele ya wanafunzi waliohudhuria katika mkutano huo, Mwenyekiti wa UDOMSSO ndugu James Simon aliueleza mkutano juu ya malengo, mipango, mafanikio na changamoto zinazoikabili UDOMSSO ambapo mbali na mafanikio mbalimbali, amesema UDOMSSO inakabiliwa na uhaba wa pesa za kuiendeshea na kufanya shughuli mbalimbali za kimasomo na kijamii. "Organization inajiendesha kwa kutegemea pesa za michango yenu nyie wanafunzi, hasa ada zenu za uanachama; hivyo nawaombeni sana wanafunzi wote ambao hamjatoa ada zenu za uanachama mlipe ili tuweze kuwa na pesa za kutosha za kuendeshea organization na kutimiza malengo na mipango organization iliyojiwekea", alisema mwenyekiti.
Katibu mkuu wa UDOMSSO, ndugu Stanley Mellack

Aidha, Katibu mkuu wa UDOMSSO ndugu Stanley Mellack akitoa maelezo juu ya Blog alisema kuwa Blog ina faida nyingi kwa Organization, na kwa jamii pia. Miongoni mwa faida hizo Katibu mkuu ndugu Mellack amesema kuwa UDOMSSO inaweza kujipatia kipato kupitia matangazo ya kibiashara ambayo makampuni yanaweza yakavutiwa na Blog na kuamua kutangaza biashara zao kupitia Blog hii.

Faida nyingine ni kuleta mabadiliko katika jamii ambapo amesema kuwa habari inayochapishwa kwenye blog kama ilivyo mitandao mingine ya kijamii inaweza kusaidia kuibadilisha jamii kwa nyanja mbalimbali kama vile kutoa elimu juu ya jambo fulani, kuhamasisha maendeleo, na kubadilisha mtazamo wa jamii kubwa ya watu watakaosoma machapisho ya blog hii.
Lakini pia akaongeza kuwa Blog ni nyenzo muhimu ya kuitangaza UDOMSSO mahali popote duniani kwakuwa blog inaweza kutazamwa na mtu yeyote duniani kote na kusoma machapisho (posts) yaliyopo.

Aidha katibu huyo hakusita kuzitaja athari zinazoweza kuletwa na matumizi mabaya ya blog kama vile kusababisha vurugu miongoni mwa wanajamii, uchochezi kama vile wa kisiasa na kidini,na mambo mengine yanayoweza kusababisha kutoweka kwa amani.

Kuu wa Idara ya Sosholojia Dr. Nelson Ishengoma
Pamoja na kuonesha masikitiko yake kwa uchache wa wanafunzi waliohudhuria katika kikao hicho; Mkuu wa Idara ya sosholojia na Anthropoloji amewataka wanafunzi wote wanajumuia kuwa na ushirikiano wao kwa wao na kutoa ushirikiano pia kwa viongozi wa jumuia hiyo ili iweze kusonga mbele. "Viongozi hawa mliowachagua kuiongoza organization hii hawawezi kufanikiwa au kuifanya organization iendelee kuwa hai pasipo nyinyi wanachama. Ushiriki wenu katika kupanga mikakati mbalimbali wa organization ni muhimu sana. Lakini utashiriki vipi au utaisaidia vipi organization kama hautahudhuria katika vikao kama hivi na shughuli nyingine zinazowakutanisha pamoja kama wanajumuia?", alihoji Dokta Ishengoma.  Wanafunzi wanahitaji kushirikiana vema katika masuala mbalimbali hasa ya kielimu na hata mengine ambayo kwa  namna moja ama nyingine ushiriki wa mtu mwingine waweza kuleta mafanikio katika hilo, aliongeza.

Mwenyekiti wa UDOMSSO (kulia) na Mkuu wa Idara
Akikabithiwa cheti na mwenyekiti wa organization, ambacho kilitolewa na hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma kwa kutambua mchango wa wana-sosholojia walipotoa msaada na kuchangia damu katika hospitali hiyo, mkuu wa Idara Dokta Ishengoma amewapongeza viongozi wote kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya japo katika mazingira magumu hasa ya kiuchumi na kuiweka UDOMSSO karibu na jamii. Hiki cheti ni cha wanasosholojia wote walioshiliki na ambao hawakushiriki katika tukio zima na ndiyomaana kimeandikwa UDOM SOCIOLOGISTS . Lakini ambao hawakushiriki kwa namna yoyote wajisikie aibu kuwa hawakutoa mchango wowote.

No comments:

Post a Comment