ABOUT UDOMSSO

The University of Dodoma Sociology Students' Organization (UDOMSSO) is an academic and social organization which is under the department of Sociology and Anthropology in the College of Humanities and Social Sciences.

MISSION

Our mission is to Organize, Coordinate and Facilitate all activities relating to our areas of interest for social progress.

VISSION

UDOMSSO has a vission to become an effective students' organization and to spearhead for a positive community for both academic and social matters which affect students' daily life and the community at large.

Translate

Monday, 26 February 2018

HIZI NDIZO FEDHA ZENYE THAMANI NDOGO ZAIDI DUNIANI.

Ukizungumzia thamani ya pesa, watu wengi hupenda kujua na kufuatilia zaidi fedha zenye thamani kubwa zaidi. Na hapa zitatajwa fedha kama vile Paundi ya Uingereza, Euro, Dola ya Kimarekani na nyingine zenye thamani kubwa kama hizo.

Lakini Je, unazijua fedha zenye thamani ya chini kabisa ulimwenguni? Hizi hapa ni Chache kati ya hizo.

1. RIAL ya Iran (Iranian Rial); 
Hii ndiyo fedha inayosemekana kuwa na thamani ndogo zaidi duniani kwa mwaka 2018 na hatamiaka ya hivi karibuni. Ukiwa na noti ya Dola moja ya Marekani itakuwa na thamani sawa na zaidi ya 30,000/= (elfu thelathini) za Iran. Hata fedha ya Kitanzania imeiacha mbali kwa thamani kwani ukiwa na shilingi 1,000 tu ya kibongo ni sawa na kitita cha zaidi ya 15,000/= ya Iran. Vita na tishio la silaha za nyukria ulimwenguni kutoka serikali ya Irani , kutiliwa vikwazo vya kiuchumi na kisiasa vinatajwa kuwa ni chanzo cha fedha ya nchi hiyo kuwa na thamani ndogo zaidi.

2. DOBRA ya St. Tome and Principe (Sao Tomean Dobra); 
Visiwa hivi viwili vilivyopo Afrika Magharibi fedha yake ni ya pili kwa kuwa na thamani ndogo. Pamoja na fedha yake kuwa na thamani kuliko ile ya Iran lakini bado Dola moja ya Marekani ni sawa na Dobra zaidi ya 22,600/= (elfu ishirini na mbili na mia sita). Pamoja na kusafirisha nje kahawa, cocoa na nazi lakini hii haijasaidia kuimarika kwa thamani ya pesa yao.Kugunduliwa kwa mafuta katika kisiwa cha St. Tome kunatazamiwa kuwa chachu ya kuongezeka thamani ya Dobra hivi karibuni.

3. DONG ya Kivietinam (Vietnamese Dong); 
Fedha hii ya Kivietnam nayo ina thamani ndogo japo imeimarika zaidi kuliko ya Iran na St. Tome. Dola moja ni sawa na Dong zaidi ya 22,300. Wataalam wanadai kuwa serikali ya Vietnam iko katika njia sahihi ya kuikuza thamani ya Dong.

Fedha nyingine zenye thamani ndogo duniani (kwa kufuatana) ni pamoja na:-
4.Belarusian Ruble, ambapo Dola moja ni sawa na Rubble 20,846, na 5. Indonesian Rupiah ambayo Dola moja ni sawa na Rupiah 13,873.

No comments:

Post a Comment