ABOUT UDOMSSO

The University of Dodoma Sociology Students' Organization (UDOMSSO) is an academic and social organization which is under the department of Sociology and Anthropology in the College of Humanities and Social Sciences.

MISSION

Our mission is to Organize, Coordinate and Facilitate all activities relating to our areas of interest for social progress.

VISSION

UDOMSSO has a vission to become an effective students' organization and to spearhead for a positive community for both academic and social matters which affect students' daily life and the community at large.

Translate

Wednesday, 14 March 2018

POLISI: NONDO ALIJITEKA MWENYEWE.


TSNP: TAARIFA ZA KILICHOMSIBU NONDO ZINAKINZANA.
Kamanda Mambosasa akiwa na Nondo


Dar es salaam. Jeshi la polisi kupitia kwa kwa Kamanda Mambosasa limedai kuwa mwanafunzi wa chou kikuu cha Dar es salaa (NONDO) ambaye alidaiwa kutekwa na watu wasiojulikana; hakutekwa na mtu yoyote labda alijiteka yeye mwenyewe. Taarifa za kutekwa kwa Nondo ambaye pia ni mwenyekiti wa mtandao  wa wanafunzi Tanzania zilianza kusikika hasa kwenye mitandao ya kijamii tarehe 6 Machi 2018, ambapo inadaiwa Nondo mwenyewe alimtumia ujumbe wa simu (sms) Rafiki yake usiku wa manane akidai kuwa yuko kwenye hatari kubwa (I am at high risk).

Akiongea mbele ya waandishi wa habari Kamanda Mambosasa
jana alisema kuwa uchunguzi wao (polisi) umebaini kuwa Nondo alikuwa anatafuta kiki tu kwa maslahi yake mwenyewe anayoyajua. Aidha Mambosasa alitanabaisha mbele ya waandishi wa habari kuwa, uchunguzi unaonesha kwamba kiongozi huyo wa mtandao wa wanafunzi Tanzania alienda Iringa kwa mpenzi wake. Kupitia mawasiliano ya simu ya mkononi ya Nondo, polisi iliweza kugundua kuwa baada ya kutuma ujumbe kwa Rafiki yake kuwa yuko katika hatari kubwa, Nondo aliendelea kuwasiliana na mpenzi wake huyo kitu kinachoashiria kuwa huru.

Nondo alionekana mjini Iringa akiwa hana tatizo lolote linaloonesha kupigwa au kuumizwa Kimwili na wala Nondo mwenyewe hakuripoti tukio hilo popote; si polisi wa kwa mjumbe baada ya kuachiwa huru na watekaji bali alikuwa akiendelea na shughuli zake tu mkoani hapo. Mara baada ya uchunguzi kukamilika Mambosasa alisema kuwa Nondo atapelekwa mahakamani kutokana na taarifa hizo za uongo zilizoleta taharuki mitaani.

Kwa upande mwingine mtandao wa wanafunzi nchini Tanzania umesema kuwa taarifa za nini hasa kilichomsibu Nondo zinakinzana. “Sisi bado hatuamini uchunguzi uliofanywa na polisi kwakuwa hatujamsikia Nondo akiongea; na kile kilichoelezwa na polisi mkoani Iringa na hiki tulichokisikia leo kwa polisi Dar es salaam haviendani”, alisema msemaji wa TSNP Hellen Sisya akiiambia BBC.


No comments:

Post a Comment