Anaitwa HACHIKO, ndiye mbwa anayeaminiwa kuwa na upendo
wa dhati na mtiifu kuliko mbwa wengine duniani. Alizaliwa Novemba 10, 1923
nchini Japan katika jiji la Tokyo. Umaarufu wake duniani ulitokana na heshima, upendo
wa dhati na utii kwa Bosi wake Hidesaburo Ueno aliyekuwa Profesa katika idara
ya kilimo katika chuo kikuu cha Tokyo nchini Japan.
Hachiko enzi za uhai wake |
Kila mara Hachiko alikuwa akimsindikiza Bosi wake katika kituo cha treni cha
Shibuya (Shibuya station) alipokuwa akipanda treni na kuelekea kazini. Mbwa
huyo alihakikisha Profesa Hidesaburo amepanda treni na kuondoka ndipo na yeye
anarudi nyumbani. Tofauti na wengi tusiozingatia muda; kila ilipofika jioni,
Hachiko aliwahi stesheni kumpokea Bosi wake katika kituo cha Shibuya kwani
alijua vyema muda wa treni kuwasili. Alifanya hivyo kila siku ambayo Bosi wake
alitoka kwenda kazini na kuzidi kujizolea umaarufu. Siku moja mwezi Mei 1925
alimsindikiza Bosi wake stesheni ya Shibuya kama kawaida yake bosi alipokuwa
akienda kazini. Jioni kama ilivyokuwa ada aliwahi stesheni kumpokea. Hata hivyo
treni ilipowasili,.....
abiria wote waliteremka lakini Hachiko hakumuona Bosi wake akiteremka.
abiria wote waliteremka lakini Hachiko hakumuona Bosi wake akiteremka.
![]() |
| Picha ya mwisho ya hachiko akiwa amekufa,wa pili kutoka kuliawalio chuchumaa ni mke wa Profesa Hidesaburo na baadhi ya staff wa stesheni ya Shibuya wakiomboleza. |
Alikaa
hapo stesheni kwa muda na baadaye alikata tamaa na kurudi nyumbani akiwa ni
mwenye huzuni.Siku hiyo Profesa Ueno akiwa kazini alipatwa na ugonjwa na muda
mfupi tu alifariki akiwa hukohuko kazini. Hachiko aliendelea kufika stesheni
kila jioni treni ilipowasili kuona kama atamwona Bosi wake akiteremka lakini
alirejea nyumbani peke yake. Miaka na miaka ilizidi kwenda lakini Hachiko
hakukata tamaa ya kwenda stesheni ya Shibuya kumsubiria Bosi wake kwani
aliamini ipo siku Bosi atarejea na atarudi naye nyumbani. Machi 8, 1935 Hachiko
alifariki dunia akiwa maeneo ya stesheni msubiri Bosi wake Profesa Hidesaburo
Ueno ikiwa ni miaka karibia 10 tangu afariki dunia. Baadaye madaktari walitoa
taarifa kuwa Hachiko alikufa kwa ugonjwa wa kansa. Hachiko alileta simanzi
miongoni mwa watu waliokuwa wakifuatilia maisha yake. Lilijengwa sanamu la
Hachiko hapo stesheni ya Shibuya, pia ulijengwa mnara wa Hachiko pembezoni mwa
kaburi la Profesa Ueno lililopo katika makaburi ya Aoyama.

No comments:
Post a Comment