ABOUT UDOMSSO

The University of Dodoma Sociology Students' Organization (UDOMSSO) is an academic and social organization which is under the department of Sociology and Anthropology in the College of Humanities and Social Sciences.

MISSION

Our mission is to Organize, Coordinate and Facilitate all activities relating to our areas of interest for social progress.

VISSION

UDOMSSO has a vission to become an effective students' organization and to spearhead for a positive community for both academic and social matters which affect students' daily life and the community at large.

Translate

Friday, 8 September 2017

TUNDU LISU AHAMISHIWA NAIROBI, AFYA YAKE INATIA MOYO


Tundu Lisu

Tukio la kupigwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Antipas Lissu (Chadema) na watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwake jana mchana limeendelea kulaaniwa vikali na watu mbalimbali wakiwemo wanasiasa, viongozi wa dini na wananchi mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii na media nyinginezo.

Lissu akiwa amefika nyumbani kwake Area D, eneo la Site Three, baada ya kuahirishwa kwa kikao cha bunge, kabla hajashuka kwenye gari watu wasiojulikana wakiwa kwenye gari linalodaiwa kuwa ni aina ya Nisani ambalo namba zake hazikutambulika, walianza kumshambulia kwa risasi.

Kwa mujibu wa ripoti ya Kamanda wa Polisi Dodoma, Gilles Muroto, risasi
zilizotumika ni kati ya 28 mpaka risasi 32. Risasi kadhaa zilimpata kwenye mwilini, mkononi risasi moja, miguuni risasi mbili na tumboni risasi mbili, kwa hiyo jumla risasi tano zilimjeruhi. Baada ya tukio watu hao walikimbia.

“Lissu alikimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa kutumia gari la familia ya Naibu Spika kwa kuwa wanaishi jirani. Alipofikishwa aliingizwa kwenye chumba cha upasuaji na kufanyiwa upasuaji kuzuia damu kuendelea kuvuja, ambapo Katibu MKuu wa Wizara ya Afya aliongoza upasuaji huo kwa kushirikiana na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma.

Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ulikuwa umeagiza ndege kwa ajili ya kumchukua mgonjwa kumpeleka Muhimbili. Lakini familia na Mwenyekiti wa chadema Freeman Mbowe, walishauri apelekwe hospitali ya Aga-Khan, Nairobi nchini Kenya kwa matibabu zaidi.
Aidha, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Vincent Mashinji amesema kuwa amepokea taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe kuwa Tundu Lissu amezinduka leo asubuhi na kwa sasa anajitambua na anaendelea vizuri.

No comments:

Post a Comment